99久久国产综合色|国产精品,日韩AV一级特黄无码人妻,91在线视频无码,国产网站久章草在线视频

Marais wa China na Russia wafanya mazungumzo

(Tovuti ya Gazeti la Umma) Septemba 03, 2025

(Picha/Xinhua)

(Picha/Xinhua)

Rais Xi Jinping wa China Jumanne amefanya mazungumzo na rais wa Russia Vladimir Putin, ambaye yupo ziarani nchini China kuhudhuria Mkutano wa viongozi wa Jumuiya ya Ushirikiano ya Shanghai (SCO) wa mwaka 2025, na Maadhimisho ya miaka 80 ya ushindi wa vita vya watu wa China dhidi ya uvamizi ya Japan na ushindi wa vita vya dunia vya kupinga ufashisti.

Katika mazungumzo hayo, rais Xi amesisitiza kuwa China na Russia zina msukumo mkubwa wa kujiendeleza, na kwamba zinatakiwa kuongeza uthabiti wa ushirikiano na kuimarisha na kulinda hali ya jumla ya ushirikiano.

Kwa upande wake rais Putin amesema Russia iko tayari kudumisha ushirikiano wa kimkakati na China, kuimarisha mawasiliano ya viongozi wa ngazi ya juu na kuongeza ushirikiano wa kiutendaji katika sekta mbalimbali, ili kukuza maendeleo ya kiwango cha juu ya uhusiano kati ya nchi hizo mbili.

(Wahariri wa tovuti:Song Ge,Zhao Jian)

Picha