99久久国产综合色|国产精品,日韩AV一级特黄无码人妻,91在线视频无码,国产网站久章草在线视频

Sudan yakaribisha hatua ya UNSC kukataa mamlaka ya pamoja

(CRI Online) Machi 07, 2025

Serikali ya Sudan siku ya Alhamisi ilikaribisha taarifa ya Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa (UNSC) ya kukataa kutiwa saini mkataba unaolenga kuunda mamlaka ya pamoja nchini humo.

Kupitia taarifa ya waziri wa habari wa Sudan ambaye pia ni msemaji wa serikali, Khalid Ali Aleisir, amesisitiza azma ya serikali ya kutafuta suluhu ambazo zitahakikisha mgogoro huo unamalizika, kulinda umoja na ukamilifu wa ardhi ya Sudan, na kutimiza matarajio ya watu wake ya kuwepo kwa usalama, demokrasia na maendeleo.

Aidha amesisitiza umuhimu wa ushirikiano wa kimataifa katika kusaidia walioathirika na vita akisisitiza dhamira ya serikali katika kuwezesha utoaji wa misaada ya kibinadamu.

Siku ya Jumatano katika taarifa UNSC ilieleza "wasiwasi mkubwa" juu ya kutiwa saini kwa mkataba wa kuanzisha mamlaka ya pamoja nchini Sudan.

(Wahariri wa tovuti:Song Ge,Zhao Jian)

Picha