99久久国产综合色|国产精品,日韩AV一级特黄无码人妻,91在线视频无码,国产网站久章草在线视频

Ufaransa yakabidhi rasmi kambi ya kijeshi ya Port Boué kwa Cote d'Ivoire

(CRI Online) Februari 21, 2025

Waziri wa Ulinzi wa Ufaransa Sébastien Lecornu na Waziri wa Ulinzi wa Cote d'Ivoire Téné Birahima Ouattara kwa pamoja wamesaini hati ya makabidhiano jana Alhamisi katika Bandari ya Bouet mjini Abidjan, ambapo Ufaransa imekabidhi rasmi kituo cha kijeshi cha Bandari ya Bouet kwa Cote d'Ivoire.

Mapema siku hiyo, Ufaransa kwanza ilikabidhi kambi ya Kikosi cha 43 cha Wanamaji wa Ufaransa, ambayo awali ilikuwa kwenye kituo cha kijeshi cha Bandari ya Bouet, kwa jeshi la Cote d'Ivoire.

Kwa mujibu wa ripoti za vyombo vya habari vya nchi hiyo, C?te d'Ivoire itakipa kituo hicho cha kijeshi cha Port Bouet jina la Mnadhimu Mkuu wa kwanza jeshi la nchi hiyo baada ya uhuru wake.

(Wahariri wa tovuti:Zhou Linjia,Zhao Jian)

Picha