99久久国产综合色|国产精品,日韩AV一级特黄无码人妻,91在线视频无码,国产网站久章草在线视频

Umoja wa Afrika watoa wito wa kusimamishwa mara moja kwa mapigano mashariki mwa DRC

(CRI Online) Februari 20, 2025

Umoja wa Afrika (AU) umetoa wito wa kusimamishwa mara moja bila ya masharti kwa mapigano na kundi la waasi wa M23 na makundi mengine yenye silaha kuondoka haraka mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC).

Kauli hiyo imetolewa na Baraza la Amani na Usalama la Umoja huo katika taarifa iliyotolewa Jumanne wiki ya wiki hii kufuatia mkutano wake wa hivi karibuni kuhusu kuongezeka kwa mapigano katika eneo hilo la mashariki mwa DRC.

Baraza hilo huku likieleza wasiwasi mkubwa kuhusu hali ya usalama na kibinadamu inayoendelea kuwa mbaya mashariki mwa DRC, limesema hali hiyo inahitaji hatua za pamoja katika moyo wa "Masuluhisho ya Afrika kwa matatizo ya Afrika.”

Pia Baraza hilo limeeleza umuhimu wa kutafuta chanzo halisi cha mgogoro huo, ikiwemo matumizi yasiyo halali ya rasilimali za asili, na kuahidi kuendelea na juhudi za kutatua mgogoro huo.

(Wahariri wa tovuti:Song Ge,Zhao Jian)

Picha