99久久国产综合色|国产精品,日韩AV一级特黄无码人妻,91在线视频无码,国产网站久章草在线视频

Kenya yaimarisha hatua za kuzuia kuenea kwa magonjwa yanayoambukizwa na?virusi

(CRI Online) Februari 13, 2025

Mamlaka ya afya ya Kenya imesema kuwa hatua madhubuti zinaendelea kuchukuliwa ili kupunguza hatari za magonjwa yanayoambukizwa na virusi kama vile Marburg, mpox, na Ebola kote nchini humo.

Waziri wa Afya wa nchi hiyo Deborah Barasa amesema siku ya Jumatano kwamba ingawa mlipuko wa virusi vya Marburg bado umedhibitiwa katika Mkoa wa Kagera, Tanzania, lakini ukaribu wa kijiografia wa Kenya na mwingiliano mkubwa wa mipaka unasababisha hatari kubwa ya watu wenye virusi hivyo kuingia nchini humo.

Barasa amesema Wizara ya Afya, kwa kushirikiana na Shirika la Afya Duniani (WHO) na washirika wengine, imeongeza hatua za ufuatiliaji na mwitikio ili kuhakikisha kuwa kuna maandalizi endelevu.

Ameongeza kuwa juhudi pia zinaendelea kuwezesha upatikanaji wa chanjo dhidi ya mpox kupitia ushirikiano na WHO na Vituo vya Afrika vya Kudhibiti na Kuzuia Magonjwa.

(Wahariri wa tovuti:Zhou Linjia,Zhao Jian)

Picha