99久久国产综合色|国产精品,日韩AV一级特黄无码人妻,91在线视频无码,国产网站久章草在线视频

Chama cha upinzani cha Sudan Kusini chapinga kufutwa kazi serikalini kwa maafisa?wake

(CRI Online) Februari 13, 2025

Chama cha upinzani cha Sudan Kusini cha Sudan People's Liberation Movement-in-Opposition (SPLM-IO), kinachoongozwa na Makamu wa Kwanza wa Rais Riek Machar, kimetoa wito wa kurejeshwa kazini kwa maafisa wawili wa chama hicho ambao walitimuliwa kwenye serikali ya mpito ya umoja wa kitaifa na Rais Salva Kiir.

Waziri wa Afya Yolanda Awel Deng, na Gavana wa Jimbo la Ikweta Magharibi Alfred Futuyo Karaba ni miongoni mwa maafisa tisa waliofutwa kazi chini ya amri ya rais iliyosomwa kwenye Shirika la Utangazaji la Sudan Kusini.

Katika taarifa yake hiyo siku ya Jumatano, Machar amekataa kile alichokiita "uamuzi wa upande mmoja" wa rais kuwafuta kazi maafisa hao, akikiuka Mkataba wa Amani wa 2018, ambao pamoja na mambo mengine umeweka sharti la kufanya maamuzi ya pamoja kati ya pande zilizotia saini kabla ya kufanya mabadiliko makubwa ndani ya serikali ya mpito ya umoja wa kitaifa.

(Wahariri wa tovuti:Zhou Linjia,Zhao Jian)

Picha