99久久国产综合色|国产精品,日韩AV一级特黄无码人妻,91在线视频无码,国产网站久章草在线视频

WHO laonya kuhusu ongezeko la kasi la maambukizi ya malaria nchini Ethiopia

(CRI Online) Desemba 25, 2024

Ripoti iliyotolewa na Shirika la Afya Duniani (WHO) Jumatatu wiki hii imesema maambukizi milioni 8.4 ya malaria yameripotiwa nchini Ethiopia tangu mwanzoni mwa mwaka huu, na ugonjwa huo unaendelea kuhatarisha afya ya umma nchini humo ambapo kwa wastani maambukizi laki 3 ya ugonjwa huo yanaripotiwa kila wiki, karibu kila eneo la nchi hiyo limeripoti maambukizi ya ugonjwa huo.

Malaria ni ugonjwa unaoenea zaidi katika maeneo yaliyo chini ya mwinuko wa mita 2,000 nchini Ethiopia, yakijumuisha robo tatu ya ardhi ya nchi hiyo, na takriban asilimia 69 ya watu wa nchi hiyo wanaoishi katika maeneo hayo wanakabiliwa na hatari ya kuambukizwa.

(Wahariri wa tovuti:Song Ge,Zhao Jian)

Picha