99久久国产综合色|国产精品,日韩AV一级特黄无码人妻,91在线视频无码,国产网站久章草在线视频

Umoja wa Afrika wakaribisha makubaliano kati ya Ethiopia na Somalia kuhusu mzozo wa Somaliland

(CRI Online) Desemba 13, 2024

Mwenyekiti wa Kamisheni ya Umoja wa Afrika (AU) Moussa Faki Mahamat amekaribisha makubaliano ya hivi karibuni yaliyosainiwa na viongozi wa Ethiopia na Somalia kuhusu mgogoro wa Somaliland, eneo lililojitangaza kujitenga la Somalia.

Ethiopia na Somalia zilifikia makubaliano siku ya Jumatano baada ya mazungumzo ya upatanishi ya Uturuki mjini Ankara, ikiashiria mafanikio katika kutatua sintofahamu kati ya nchi hizo mbili.

Mvutano umekuwa ukiongezeka kati ya Ethiopia na Somalia baada ya Ethiopia na Somaliland kusaini makubaliano mapema mwaka huu ya kuruhusu Ethiopia kufikia Bahari ya Sham kwa kuitambua Somaliland kama taifa huru.

Somalia, ambayo inaichukulia Somaliland kuwa sehemu ya ardhi yake, ilielezea makubaliano hayo kuwa hayana nguvu za kisheria.

Kufuatia makubaliano hayo, Waziri Mkuu wa Ethiopia Abiy Ahmed na Rais wa Somalia Hassan Sheikh Mohamud walitoa taarifa ya pamoja wakisisitiza ushirikiano na mazungumzo kati ya nchi hizo mbili.

Viongozi wote wawili wamesisitiza kuheshimiana kwenye utawala, umoja, uhuru, na mamlaka ya nchi na kukubaliana kushirikiana ili kukamilisha mipango ambayo itawezesha Ethiopia kuingia na kutoka baharini.

(Wahariri wa tovuti:Zhou Linjia,Zhao Jian)

Picha