99久久国产综合色|国产精品,日韩AV一级特黄无码人妻,91在线视频无码,国产网站久章草在线视频

Madaktari wa China watoa huduma bila malipo katika kuadhimisha Siku ya Kunawa Mikono

(CRI Online) Desemba 10, 2024

(Picha inatoka tovuti ya CRI)

Timu ya wataalam wa matibabu wa China imetoa elimu ya afya na huduma za matibabu bila malipo katika Visiwa vya Pemba nchini Tanzania ikiwa ni sehemu ya maadhimisho ya Siku ya Kunawa Mikono Duniani mwaka huu.

Shughuli hiyo iliyofanyika katika Shule ya Sekondari Kiwani na Kitengo cha Zahanati ya Afya ya Msingi, iliongozwa na kundi la pili la wataalam wa Mradi wa Msaada wa Kudhibiti na Kutokomeza Ugonjwa wa Kichocho kutoka China na Zanzibar na Kundi la 34 la Timu ya Madaktari wa China iliyopo Pemba.

Huduma hiyo, ambayo imevutia wakazi na wanafunzi wenyeji zaidi ya 400, imefanywa kwa ushirikiano na wawakilishi kutoka idara za afya na elimu na Kitengo cha Programu ya Magonjwa ya Kitropiki Yaliyosahaulika (NTD) visiwani Zanzibar.

(Picha inatoka tovuti ya CRI)

(Picha inatoka tovuti ya CRI)

(Wahariri wa tovuti:Song Ge,Zhao Jian)

Picha