99久久国产综合色|国产精品,日韩AV一级特黄无码人妻,91在线视频无码,国产网站久章草在线视频

Vyombo vya habari vya Russia vyasema Bashar al-Assad amewasili Moscow

(CRI Online) Desemba 09, 2024

Habari kutoka Shirika la Habari la Russia, TASS imesema aliyekuwa rais wa Syria, Bashar al-Assad na familia yake wamewasili Moscow nchini Russia, ambapo nchi hiyo imewapa hifadhi.

Kundi la upinzani la Syria limetangaza jana Jumapili, Desemba 8 kuwa limeingia Damascus, mji mkuu wa nchi hiyo na kupitia televisheni likasema kuwa limeikomboa Damascus na kupindua serikali ya al-Assad.

Wizara ya mambo ya nje ya Russia imetoa taarifa siku hiyo ikisema baada ya kufanya mazungumzo na pande zote za mapigano nchini Syria na kuagiza kukabidhi madaraka kwa amani, Bashar al-Assad ameamua kujiuzulu wadhifa wa urais wa Syria na kuondoka nchini humo.

Likinukuu taarifa kutoka Ikulu ya Russia, Klemrin, Shirika la TASS limesema kuwa Russia imewapa Bashar al-Assad na familia yake hifadhi kutokana na sababu ya kibinadamu.

Taarifa hiyo imeongeza kuwa, Russia inaunga mkono siku zote kutafuta suluhu ya kisiasa kwa mgogoro wa Syria, na madhumuni ya Russia ni kurejesha mazungumzo chini ya upatanishi wa Umoja wa Mataifa.

(Wahariri wa tovuti:Zhou Linjia,Zhao Jian)

Picha