99久久国产综合色|国产精品,日韩AV一级特黄无码人妻,91在线视频无码,国产网站久章草在线视频

Kenya yazindua mfumokazi wa kuboresha uchumi wa kazi za vibarua

(CRI Online) Novemba 13, 2024

Kenya imezindua mfumokazi mpya kwa ajili ya kuandaa dira ya kisera ili kuhimiza uchumi wake wa kazi za vibarua.

Katibu Mkuu wa Wizara ya Habari, Mawasiliano na Uchumi wa Kidigitali ya Kenya, Bibi Mary Kerema amesema mfumokazi huo wenye kichwa cha "mwongozo wa kisera kwa maendeleo ya uchumi wa kidijitali," unatoa dira jumuishi ya kuboresha uchumi wa ajira zisizo za kudumu nchini Kenya na kuunda sekta yenye usawa na endelevu zaidi kwa wafanyakazi zaidi ya milioni moja na biashara zinazotokana na kazi hizo.

“Mfumokazi huo unatoa sera ya kina kama mwongozo wa kukuza uchumi wa kidijitali nchini Kenya” amesema Bibi Kerema kwenye hafla ya uzinduzi wa mfumokazi huo.

Amebainisha kuwa mfumokazi huo utaanzisha mikakati mipya inayolenga kupanua ufikiaji wa huduma za kidijitali na kuhimiza ukuaji endelevu wa uchumi wa kidijitali.

(Wahariri wa tovuti:Zhou Linjia,Zhao Jian)

Picha