99久久国产综合色|国产精品,日韩AV一级特黄无码人妻,91在线视频无码,国产网站久章草在线视频

Mtaalamu wa Kenya asema biashara na China imeboresha ustawi wa maisha ya Waafrika

(CRI Online) Novemba 04, 2024

Biashara inayoshamiri kati ya nchi za Afrika na China imesaidia katika upatikanaji wa nafasi za ajira na kuinua kiwango cha maisha katika nchi za Afrika.

Hayo yamesemwa na mchumi wa Kenya Profesa Xn Iraki wa Chuo Kikuu cha Nairobi cha Kenya alipohojiwa na Shirika la Habari la China, Xinhua. Profesa Iraki amesisitiza nafasi muhimu ya usawa wa kibiashara kama msingi wa kunufaishana, na kuchochea maendeleo ya kasi barani Afrika na China.

Profesa Iraki pia amesisitiza umuhimu wa majukwaa ya majadiliano kati ya China na nchi za Afrika, kama vile Baraza la Ushirikiano kati ya China na Afrika (FOCAC), ambayo yanachukua nafasi muhimu kama njia ya kutimiza maslahi ya pamoja, kukabiliana na changamoto za kibiashara, na kutumia fursa ambazo bado hazijatumika.

Pia amependekeza uhusiano wa uwazi kati ya wafanyabiashara wa pande hizo mbili na kutafiti maeneo mapya ya kibiashara bila kujali umbali wa kijiografia kati ya China na nchi za Afrika.

(Wahariri wa tovuti:Zhou Linjia,Renato Lu)

Picha