99久久国产综合色|国产精品,日韩AV一级特黄无码人妻,91在线视频无码,国产网站久章草在线视频

Tunisia, Iraq zaahidi kuimarisha ushirikiano wa kitamaduni

(Tovuti ya Gazeti la Umma) Septemba 20, 2024

Rais wa Tunisia Kais Saied (Kulia) akikutana na Waziri wa Utamaduni, Utalii na Mambo ya Kale wa Iraq Ahmed Fakak Al-Badrani mjini Tunis, Tunisia, Septemba 19, 2024. (Urais wa Tunisia/Kitini kupitia Xinhua)

Rais wa Tunisia Kais Saied (Kulia) akikutana na Waziri wa Utamaduni, Utalii na Mambo ya Kale wa Iraq Ahmed Fakak Al-Badrani mjini Tunis, Tunisia, Septemba 19, 2024. (Urais wa Tunisia/Kitini kupitia Xinhua)

TUNIS - Rais wa Tunisia Kais Saied ametangaza Alhamisi kwenye mkutano na Waziri wa Utamaduni, Utalii, na Mambo ya Kale wa Iraq Ahmed Fakak Al-Badrani kwamba Tunisia iko tayari kuimarisha ushirikiano wa kitamaduni na Iraq.

Kwa mujibu wa ikulu ya Tunisia, kwenye mkutano huo, Saied amesisitiza dhamira ya Tunisia ya kuimarisha mabadilishano ya kitamaduni na kuendeleza mifumo ya ushirikiano wa pande mbili, hasa kwa kuanzisha vituo vya kitamaduni katika pande zote za Tunisia na Iraq.

Amesisitiza zaidi umuhimu wa utamaduni katika kuendeleza fikra za kiufunuo na kupambana na itikadi kali, akisema kwamba "utamaduni ni ngome ya jamii na daraja la kizuoni la ukaribu kati ya watu."

Kwa upande wake, Al-Badrani ameelezea shauku ya Iraq ya kuendeleza uhusiano wa pande mbili kwa manufaa ya mataifa yote mawili.

(Wahariri wa tovuti:Zhou Linjia,Zhao Jian)

Picha