99久久国产综合色|国产精品,日韩AV一级特黄无码人妻,91在线视频无码,国产网站久章草在线视频

Kenya yaadhimisha Siku ya Tiba ya Jadi ya Afrika kwa kutoa wito wa kutambuliwa kwa tiba hiyo

(CRI Online) Septemba 02, 2024

Siku ya Tiba ya Jadi ya Afrika mwaka 2024 imeadhimishwa katika jiji la Nairobi nchini Kenya jumamosi iliyopita na kutoa wito wa kujumuisha tiba ya jadi katika mfumo mkuu wa matibabu.

Watunga sera, wanasayansi, na wataalamu wa tiba ya jadi walishiriki kwenye shughuli za siku hiyo iliyookuwa na kaulimbiu ya “Kuunga mkono upatikanaji wa tiba bora na salama ya jadi kupitia mfumo sahihi wa usimamizi.”

Mkuu wa Idara ya Dawa Mbadala na za Asili katika Wizara ya Afya nchini Kenya Pauline Duya amesema, Kenya imejizatiti kuboresha matumizi ya dawa hizo katika tiba na udhibiti wa magonjwa sugu.

Siku ya Tiba za Asili barani Afrika inaadhimishwa kila Agosti 31, na inalenga kutambua nafasi muhimu ya dawa za asili katika kudumisha mahitaji ya afya ya msingi, ikiwemo kutibu magonjwa ya kuambukiza na yasiyo ya kuambukiza.

(Wahariri wa tovuti:Song Ge,Zhao Jian)

Picha