99久久国产综合色|国产精品,日韩AV一级特黄无码人妻,91在线视频无码,国产网站久章草在线视频

China yasema maendeleo endelevu ni msingi wa amani ya kudumu barani Afrika

(CRI Online) Agosti 13, 2024

Mjumbe wa kudumu wa China katika Umoja wa Mataifa Balozi Fu Cong amesema, kazi ya msingi katika kukabiliana na historia ya udhalimu barani Afrika ni kuziunga mkono nchi za Afrika katika njia ya maendeleo endelevu kama msingi wa amani ya kudumu.

Balozi Fu amesema hayo katika mjadala wa wazi wa Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa uliofanyika jana kuhusu “Kushughulikia Historia ya Udhalimu na Kuimarisha Uwakilishi Madhubuti wa Afrika katika Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa.”

Balozi Fu amesema ili kuondokana na ukosefu wa usawa kwa bara la Afrika, jamii ya kimataifa inapaswa kupinga bila kusita urithi wa ukoloni na aina zote za vitendo vya kidhalimu, na nchi za Magharibi zinapaswa kubeba wajibu wao kihalisi wa kihistoria, kubadili mwelekeo wao, kuacha kuingilia mambo ya ndani ya nchi hizo na kurejesha mustakabali wa siku za baadaye wa Afrika kwa Waafrika wenyewe.

(Wahariri wa tovuti:Song Ge,Zhao Jian)

Picha