99久久国产综合色|国产精品,日韩AV一级特黄无码人妻,91在线视频无码,国产网站久章草在线视频

China yatoa dola milioni 3 kwa shirika la Umoja wa Mataifa ili kutoa msaada kwa Gaza

(Tovuti ya Gazeti la Umma) Agosti 05, 2024

RAMALLAH - China imechangia imetoa michango ya dola milioni 3 za Kimarekani siku ya Alhamisi kwa Shirika la Umoja wa Mataifa la mradi wa utoaji msaada kwa Wakimbizi wa Palestina katika Mashariki ya Karibu (UNRWA) ili kuunga mkono juhudi zake za dharura za kibinadamu katika Ukanda wa Gaza.

Zeng Jixin, mkuu wa Ofisi ya Jamhuri ya Watu wa China katika Taifa la Palestina, amesaini makubaliano hayo ya utoaji michango na Naibu Kamishna Mkuu (Uungaji Mkono wa Operesheni) wa UNRWA Antonia Marie De Meo, ofisi hiyo imesema katika taarifa yake.

China siku zote inaunga mkono utendaji kazi wenye ufanisi wa UNRWA, na kutoa wito kwa jumuiya ya kimataifa kuunga mkono kazi ya shirika hilo, Zeng amesema, akiongeza kuwa China ilitoa msaada wa dharura wa fedha taslimu kwa shirika hilo baada ya kuzuka kwa mgogoro wa Gaza mwaka jana.

Zeng amesema, China itaendelea kutekeleza Pendekezo la Usalama wa Dunia nzima na kushirikiana na jumuiya ya kimataifa kumaliza mapema mapigano katika eneo la Gaza, kupunguza hali mbaya ya kibinadamu na kutekeleza suluhu ya nchi mbili.

De Meo, akiwa kwa niaba ya UNRWA, ameelezea shukrani zake kwa uungaji mkono wa siku zote wa China, na kusema kwamba mchango huo wa China ni muhimu sana.

Pia ameeleza nia ya kuimarisha ushirikiano na China ili kupunguza msukosuko wa hali ya ubinadamu katika Ukanda wa Gaza.?

(Wahariri wa tovuti:Song Ge,Renato Lu)

Picha