99久久国产综合色|国产精品,日韩AV一级特黄无码人妻,91在线视频无码,国产网站久章草在线视频

Kenya yalenga kuwezesha vijana kwa sayansi, teknolojia ili kuchochea maendeleo

(CRI Online) Julai 24, 2024

Wizara ya Elimu ya Kenya imesema inadhamiria kutumia sayansi, teknolojia na uvumbuzi ili kuwezesha vijana na kuchochea maendeleo nchini humo.

Hayo yamesemwa na Katibu Mkuu wa Wizara ya Elimu ya Kenya, Beatrice Inyangala kwenye kongamano la ushiriki wa wadau wa tamasha la utafiti mjini Nairobi. Amesema serikali inatoa kipaumbele kwa utafiti na ubunifu ili kutatua changamoto nyingi za kijamii.

Amesema serikali imeanzisha ushirikiano na washirika wa ndani na kimataifa ili kuendeleza ubora wa utafiti katika taasisi zote za elimu.

Ameongeza kuwa Kenya inajifunza uzoefu mzuri kutoka nchi za China, Korea Kusini, Malaysia na Singapore, ili kuchochea ukuaji wa nchi hiyo kwa njia ya kisayansi na uvumbuzi.

(Wahariri wa tovuti:Song Ge,Zhao Jian)

Picha