99久久国产综合色|国产精品,日韩AV一级特黄无码人妻,91在线视频无码,国产网站久章草在线视频

Pembe ya Afrika kuwa na joto kali kuliko kawaida katika kipindi cha miezi ya Agosti hadi Oktoba

(CRI Online) Julai 22, 2024

Kituo cha Utabiri wa Hali ya Hewa (ICPAC) cha Shirika la Kiserikali kwa Maendeleo la Nchi za Afrika Mashariki (IGAD) kimesema eneo la Pembe ya Afrika litakuwa na halijoto kali kuliko kawaida wakati wa msimu wa kipindi cha miezi ya Agosti mpaka Oktoba.

Kituo hicho kimesema, halijoto katika baadhi ya nchi za eneo hilo inaweza kupanda hadi nyuzi joto 35, na kwamba halijoto za kawaida hadi zile zenye baridi kuliko kawaida itashuhudiwa katika baadhi ya maeneo ya Sudan mashariki na maeneo ya karibu ya Ethiopia na Eritrea.

Licha ya viwango vya juu vya joto, ICPAC imesema, maeneo ya mashariki ya Pembe ya Afrika yanatarajiwa kuwa makavu kuliko kawaida wakati wa msimu wa kipindi cha miezi ya Agosti hadi Oktoba, huku maeneo ya kaskazini yakipata mvua kubwa kuliko kawaida.

(Wahariri wa tovuti:Song Ge,Deng Jie)

Picha