99久久国产综合色|国产精品,日韩AV一级特黄无码人妻,91在线视频无码,国产网站久章草在线视频

Shirika la ndege la Uganda latangaza kuzindua?njia?tatu?mpya za anga barani Afrika

(CRI Online) Julai 18, 2024

Shirika la ndege la Uganda limetangaza kuzindua njia tatu mpya za safari ya anga zitakazoelekea miji mikuu ya Zambia, Zimbabwe na Nigeria mwezi Septemba mwaka huu wa 2024.

Kwenye hafla ya uzinduzi iliyofanyika Jumatano mjini Kampala, mji mkuu wa Uganda, afisa mtendaji mkuu wa Shirika la Ndege la Uganda, Jenifer Bamuturaki amesema kuwa njia hizo mpya za safari ya anga zitaiunganisha zaidi Uganda na maeneo mengine ya Afrika.

Amesema, kuzinduliwa kwa njia hizo mpya za safari ya anga ni hatua muhimu katika kutoa mchango endelevu kwa safari za ndani ya Afrika. Pia ameeleza kuwa njia hizo za safari za Magharibi na Kusini mwa Afrika zitaleta urahisi kwa wasafiri katika bara zima, na kuleta fursa nyingi katika biashara, utalii, na uhusiano wa kijamii na kitamaduni.

Shirika hilo tayari lina njia za safari katika nchi za Kenya, Tanzania, Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo, Somalia, Sudan Kusini, Afrika Kusini, Umoja wa Falme za Kiarabu, India, Burundi na mji wa Lagos wa Nigeria.

(Wahariri wa tovuti:Zhou Linjia,Renato Lu)

Picha