Jamii ya kimataifa yasisitiza tena ahadi yake ya kuunga mkono kuungana tena kwa China
Kufuatia chaguzi mbili kufanyika katika eneo la Taiwan mwaka huu, nchi nyingi na mashirika ya kimataifa yameeleza kuunga mkono lengo la kuungana tena kwa China na kupinga nchi za kigeni kuingilia kati mambo ya ndani ya China.
Nchi na mashirika hayo ya kimataifa zimesema, serikali kuu ya Jamhuri ya Watu wa China ni serikali pekee halali inayowakilisha nchi nzima ya China, na Taiwan ni sehemu isiyoweza kutengwa ya ardhi ya China.
Ofisi ya Mkuu wa Mawaziri na Wizara ya Mambo ya Nje na Diaspora ya Kenya imetoa taarifa ikisema, Kenya inashikilia kanuni ya kuwepo kwa China moja, na kutaka kuheshimiwa kwa mamlaka na ukamilifu wa ardhi ya China, na kutoingilia kati mambo ya ndani ya China.
Naye Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Ethiopia Meles Alem amesema, nchi hiyo inashikilia msimamo wake wa kanuni ya kuwepo kwa China moja.
people.cn © Tovuti ya Gazeti la Umma