99久久国产综合色|国产精品,日韩AV一级特黄无码人妻,91在线视频无码,国产网站久章草在线视频

China yapinga vikali Marekani kupitisha sheria kuhusu suala la Taiwan

(CRI Online) Januari 17, 2024

Msemaji wa wizara ya mambo ya nje wa China Bi. Mao Ning amesema China inapinga vikali Marekani kupitisha kile inachoita sheria inayohusiana na Taiwan, na imetoa malalamiko makali kwa upande wa Marekani.

Kwa mujibu wa habari zilizoripotiwa, Baraza la Wawakilishi la Marekani hivi majuzi lilipitisha Sheria ya Kutobagua ya Taiwan ya 2023, inayomtaka Waziri wa Fedha wa Marekani kutumia ushawishi wa Marekani katika Shirika la Fedha la Kimataifa (IMF) kuunga mkono uanachama wa Taiwan katika shirika hilo.

Akijibu swali linalohusiana na suala hilo, Bi. Mao amesema Marekani kupitisha sheria hiyo ni kitendo cha kuingilia mambo ya ndani ya China na kujaribu kutumia suala la Taiwan kwa madhumuni ya kisiasa kwa lengo la kuwa na "China mbili" yaani "China moja, Taiwan moja". China inapinga vikali na imetoa malalamiko makali kwa upande wa Marekani.

(Wahariri wa tovuti:Zhou Linjia,Zhao Jian)

Picha