99久久国产综合色|国产精品,日韩AV一级特黄无码人妻,91在线视频无码,国产网站久章草在线视频

Mkutano wa masoko ya hisa ya Afrika kuongeza biashara ya kuvuka mipaka kwa mitaji ya masoko

(CRI Online) Novemba 24, 2023

Wawakilishi wa masoko ya hisa barani Afrika wamekutana katika mkutano wa siku mbili ulioanza Alhamisi jijini Nairobi, Kenya, kwa lengo la kuongeza biashara ya kuvuka mipaka kwa kampuni zilizoorodheshwa kwenye masoko ya hisa na dhamana.

Akizungumza kwenye ufunguzi wa Mkutano wa 26 wa Mwaka wa Shirikisho la Masoko ya Dhamana na Hisa la Afrika (ASEA), Rais wa Kenya William Ruto amesema biashara ya soko la hisa na dhamana za kampuni zilizoorodheshwa kati ya nchi za Afrika itawezesha kuongeza idadi kubwa ya wawekezaji katika soko la mitaji barani humo, na kuongeza kuwa, biashara hiyo pia itawezesha nchi mbalimbali kujifunza njia bora za utenda kazi ndani ya mfumo mmoja wa kiuchumi.

Katika mkutano huo, washiriki watatafuta suluhisho thabiti la changamoto zinazoikabili sekta hiyo, na kuwezesha kuwa na mfumo wa kiuchumi wa soko la fedha la Afrika ambalo ni jumuishi na imara.

(Wahariri wa tovuti:Song Ge,Zhao Jian)

Picha