99久久国产综合色|国产精品,日韩AV一级特黄无码人妻,91在线视频无码,国产网站久章草在线视频

IMF yakadiria ukuaji wa uchumi?duniani kupungua hadi asilimia 3?Mwaka 2023 na 2024

(Tovuti ya Gazeti la Umma) Julai 26, 2023

Picha ya kumbukumbu iliyopigwa Aprili 6, 2021 ikionyesha mandhari ya nje ya makao makuu ya Shirika la Fedha la Kimataifa (IMF) mjini Washington, D.C., Marekani. (Picha na Ting Shen/Xinhua)

Picha ya kumbukumbu iliyopigwa Aprili 6, 2021 ikionyesha mandhari ya nje ya makao makuu ya Shirika la Fedha la Kimataifa (IMF) mjini Washington, D.C., Marekani. (Picha na Ting Shen/Xinhua)

NEW YORK - Ukuaji wa uchumi duniani unatarajiwa kushuka kutoka wastani wa asilimia 3.5 Mwaka 2022 hadi asilimia 3.0 Mwaka 2023 na 2024, na ukuaji wa uchumi wa China hautabadilika katika kiwango cha asilimia 5.2 Mwaka 2023 na asilimia 4.5 Mwaka 2024, limesema Shirika la Fedha la Kimataifa (IMF) siku ya Jumanne.

IMF imesema katika ripoti yake mpya ya Mtazamo wa Uchumi wa Dunia kwamba, "ingawa makadirio hayo ya Mwaka 2023 ni ya juu zaidi kuliko ilivyokadiriwa katika Mtazamo wa Uchumi wa Dunia wa Aprili 2023, bado ni dhaifu kwa kulinganishwa na viwango vya kihistoria, kupanda kwa viwango vya sera za benki kuu katika kupambana na mfumuko wa bei kunaendelea kuathiri shughuli za kiuchumi."

IMF imesema, mfumuko wa bei wa kimataifa unatarajiwa kushuka kutoka asilimia 8.7 Mwaka 2022 hadi asilimia 6.8 Mwaka 2023 na asilimia 5.2 Mwaka 2024. Mfumuko wa bei wa msingi unatarajiwa kupungua hatua kwa hatua, na makadirio ya mfumuko wa bei Mwaka 2024 yamerekebishwa kwenda juu.

Ripoti hiyo imesema, kwa nchi zilizoendelea kiuchumi, ukuaji wa uchumi unatarajiwa kushuka kwa kiwango kikubwa Mwaka 2023 -- kutoka asilimia 2.7 Mwaka 2022 hadi asilimia 1.5 Mwaka 2023.

Takriban asilimia 93 ya nchi zilizoendelea kiuchumi zinakadiriwa kuwa na ukuaji mdogo wa uchumi Mwaka 2023, na ukuaji wa Mwaka 2024 kati ya nchi hizo unatarajiwa kubaki katika asilimia 1.4, imesema ripoti hiyo.

Nchini Marekani, ukuaji wa uchumi unatarajiwa kupungua kutoka asilimia 2.1 Mwaka 2022 hadi asilimia 1.8 Mwaka 2023 na zaidi hadi asilimia 1.0 Mwaka 2024.

Ukuaji wa uchumi katika masoko yanayoibukia na nchi zinazoendelea kiuchumi unatarajiwa kuongezeka huku ukuaji wa mwaka hadi mwaka ukiongezeka kutoka asilimia 3.1 Mwaka 2022 hadi asilimia 4.1 mwaka huu na ujao.

(Wahariri wa tovuti:Zhou Linjia,Zhao Jian)

Picha