

Lugha Nyingine
Watu 9 wauawa katika shambulizi la kujitoa mhanga Kusini Magharibi mwa Pakistan
(CRI Online) Machi 07, 2023
Polisi wa Pakistan walisema, watu 9 wameuawa na wengine 10 kujeruhiwa katika shambulizi la kujitoa mhanga lililotokea jana mkoani Balochistan, kusini magharibi mwa nchi hiyo.
Polisi wamesema, mshambuliaji alipanda pikipiki iliyotegwa mabomu na kugonga lori lililobeba askari 22. Mpaka sasa hakuna kundi lolote au watu binafsi waliokiri kuhusika na shambulizi hilo.
(Wahariri wa tovuti:Zhou Linjia,Zhao Jian)
Kuhusu Tovuti ya Gazeti la Umma
people.cn © Tovuti ya Gazeti la Umma
people.cn © Tovuti ya Gazeti la Umma