99久久国产综合色|国产精品,日韩AV一级特黄无码人妻,91在线视频无码,国产网站久章草在线视频

Mwanadiplomasia Mwandamizi wa China Wang Yi akutana na mshauri wa Serikali ya Nicaragua

(Tovuti ya Gazeti la Umma) Februari 13, 2023

Wang Yi, Mjumbe wa Ofisi ya Siasa ya Kamati Kuu ya Chama cha Kikomunisti cha China (CPC) na Mkurugenzi wa Ofisi ya Kamati ya Mambo ya Nje ya Kamati Kuu ya CPC, akikutana na Laureano Ortega, mshauri wa masuala ya uwekezaji, biashara na ushirikiano wa kimataifa katika ofisi ya Rais wa Nicaragua, mjini Beijing, China, Februari 11, 2023. (Xinhua/Yao Dawei)

BEIJING - Wang Yi, Mkurugenzi wa Ofisi ya Kamati ya Mambo ya Nje ya Kamati Kuu ya Chama cha Kikomunisti cha China (CPC), Jumamosi alikutana na Laureano Ortega, mshauri wa uwekezaji, biashara na ushirikiano wa kimataifa katika ofisi ya Rais wa Nicaragua.

Wang, ambaye pia mjumbe wa Ofisi ya Siasa ya Kamati Kuu ya Chama cha Kikomunisti cha China, amepongeza maendeleo ambayo China na Nicaragua zimepata tangu kurejesha kawaida uhusiano wa kidiplomasia zaidi ya mwaka mmoja uliopita. Amesema chini ya mwongozo wa kimkakati wa viongozi wa nchi hizo mbili, ushirikiano kati ya China na Nicaragua umeendelea kwa kasi, na kuzifanya nchi hizo mbili kuwa mstari wa mbele katika uhusiano wa China na Latini Amerika.

“Kurejeshwa kwa hali ya kawaida ya uhusiano kati ya nchi hizo mbili kunaendana na mwelekeo wa historia, kunatumikia maslahi ya watu wa pande mbili na kutafungua matarajio mapana zaidi ya maendeleo ya pande zote ya mahusiano kati ya nchi hizo mbili,” amesema Wang.

Kwa upande wake Laureano Ortega amesema kuwa Nicaragua inaunga mkono kwa dhati juhudi za China za kulinda usalama wa taifa na ukamilifu wa ardhi, na inapinga kuingiliwa na nchi za nje.

Ameongeza kuwa Nicaragua inaunga mkono Pendekezo la Ukanda Mmoja, Njia Moja, Pendekezo la Maendeleo ya Dunia na Pendekezo la Usalama wa Dunia ambayo yote yanayopendekezwa na China.

(Wahariri wa tovuti:Song Ge,Zhao Jian)

Picha