99久久国产综合色|国产精品,日韩AV一级特黄无码人妻,91在线视频无码,国产网站久章草在线视频

Waziri wa Mambo ya Nje wa Ukraine asema Ukraine itafanya mkutano wa kilele wa amani msimu huu wa baridi

(Tovuti ya Gazeti la Umma) Desemba 27, 2022

KIEV - Waziri wa Mambo ya Nje wa Ukraine Dmytro Kuleba amesema Kiev inatarajia kufanya mkutano wa kilele kujadili mpango wa amani wa Ukraine ifikapo mwisho wa Februari Mwaka 2023, shirika la habari la Ukraine, Interfax limeripoti Jumatatu.

"Umoja wa Mataifa unaweza kuwa jukwaa bora zaidi la kufanya mkutano huu," Kuleba amesema, huku akipendekeza kwamba Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres atakuwa mpatanishi anayewezekana wa mazungumzo hayo ya amani.

Kuleba anaamini kuwa Russia haiko tayari kwa mazungumzo ya amani, ingawa waziri huyo amedokeza kuwa "kila vita huisha kutokana na hatua zilizochukuliwa kwenye uwanja wa vita na kwenye meza ya mazungumzo."

Akitoa maoni yake kuhusu ziara ya hivi majuzi ya Rais wa Ukraine Volodymyr Zelensky nchini Marekani, Kuleba amesema "ameridhika kabisa" na matokeo yake.

Zelensky alipendekeza na kutoa mpango wa amani wa kumaliza vita kati ya Russia na Ukraine katika mkutano wa G20 nchini Indonesia mwezi uliopita.

(Wahariri wa tovuti:Song Ge,Zhao Jian)

Picha