99久久国产综合色|国产精品,日韩AV一级特黄无码人妻,91在线视频无码,国产网站久章草在线视频

Lawama dhidi ya sera ya kibiashara ya Marekani yaonesha maoni ya pamoja ya jumuiya ya kimataifa

(CRI Online) Desemba 16, 2022

Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje ya China Wang Wenbin amesema, pande mbalimbali za Shirika la Biashara Duniani (WTO) zimepinga vitendo vya Marekani vya upande mmoja na vya kujilinda kibiashara, ikionesha maoni ya pamoja ya jumuiya ya kimataifa.

Jumatano wiki hii mjini Geneva, WTO iliitisha mkutano, ambapo China, Umoja wa Ulaya, Russia na nchi wanachama wengine zililaani vitendo vya Marekani vya kuvuruga mnyororo wa uzalishaji duniani.

Wang amesema Marekani inadai ushindani wa haki kwa sauti kubwa, lakini wakati huohuo inatoa ruzuku kubwa yenye ubaguzi, ili kusaidia kampuni zake kupata uwezo zaidi wa ushindani.

(Wahariri wa tovuti:Zhou Linjia,Zhao Jian)

Picha