99久久国产综合色|国产精品,日韩AV一级特黄无码人妻,91在线视频无码,国产网站久章草在线视频

Viongozi wa G20 wasisitiza tena ahadi ya kushirikiana katika kukabiliana na changamoto za kiuchumi duniani

(CRI Online) Novemba 17, 2022

Viongozi wa kundi la nchi 20 (G20) wamesisitiza tena ahadi yao ya kushirikiana katika kukabiliana na changamoto kubwa za kiuchumi duniani.

Kwenye azimio lililopitishwa mwishoni mwa mkutano wa 17 wa wakuu wa nchi za kundi la G20, viongozi hao wamesema watabeba jukumu kwa pamoja, na ushirikiano ni muhimu katika kufufua uchumi wa dunia, kukabiliana na changamoto na kuweka msingi wa ukuaji imara wa uchumi, ambao ni endelevu, wenye uwiano na jumuishi.

Pia wamesema ni muhimu kushikilia sheria za kimataifa na mfumo wa pande nyingi utakaolinda amani na utulivu, na kusisitiza kuwa ufumbuzi wa migogoro kwa njia ya amani, na kukabiliana na misukosuko pamoja kwa kutumia diplomasia na mazungumzo ni muhimu.

Viongozi hao pia wamesema wamedhamiria kuzisaidia nchi zinazoendelea, hasa zenye maendeleo duni na nchi za visiwa zinazoendelea, katika kukabiliana na changamoto za dunia na kufikia Lengo la Maendeleo Endelevu. 

(Wahariri wa tovuti:Song Ge,Zhao Jian)

Picha