99久久国产综合色|国产精品,日韩AV一级特黄无码人妻,91在线视频无码,国产网站久章草在线视频

Watu 32 wauawa katika shambulizi la uchomaji moto Madagascar

(CRI Online) Agosti 01, 2022

Waziri wa Ulinzi wa Taifa wa Madagascar Richard Rakotonirina amethibitisha kuwa jumla ya watu 32 wameuawa katika shambulizi la uchomaji moto lililotokea Ijumaa katika kijiji cha wilaya ya Malagasy ya Ankazobe, ambacho kiko kilomita 100 magharibi ya mji mkuu Antananarivo.

Ndege na helikopta zimehamasishwa kusaidia kuwasaka wahusika wa ukatili huu ambao umesababisha vifo vya watu thelathini na wawili, na wengine wanne kujeruhiwa.

Washambuliaji hao walijihami kwa bunduki tatu aina ya AK-47, bunduki moja aina ya MAS-36 na shotgun nane na kuchoma nyumba hiyo kutoka ghorofa ya chini. Waliwafungia wahanga na kuwapiga risasi wale waliojaribu kukimbia.

Rais Andry Rajoelina wa Madagascar ametoa rambirambi zake kwa familia za wahanga na kulaani kitendo hicho, akitangaza kuwa waliofanya uhalifu huo wanasakwa na wataadhibiwa kwa mujibu wa sheria.

(Wahariri wa tovuti:Zhou Linjia,Zhao Jian)

Picha