99久久国产综合色|国产精品,日韩AV一级特黄无码人妻,91在线视频无码,国产网站久章草在线视频

Uganda kuwa mwenyeji wa mkutano wa 63 wa Jumuiya ya Mashauriano ya Kisheria ya Asia-Afrika

(CRI Online) Septemba 02, 2025

Wawakilishi wa Serikali, wataalam wa sheria, na wajumbe wa kidiplomasia kutoka nchi wanachama 47 wanatarajiwa kukutana nchini Uganda kwa ajili ya mkutano wa 63 wa Jumuiya ya Mashauriano ya Kisheria ya Asia na Afrika (AALCO).

Mwanasheria Mkuu wa Uganda Bw. Kiryowa Kiwanuka amewaambia wanahabari kuwa mkutano huo wa siku tano uliopangwa kuanza Septemba 8, utazingatia maslahi ya nchi wanachama katika sheria za kimataifa na unalenga kueleza mitazamo ya pamoja ya kisheria ya Asia na Afrika katika jukwaa la kimataifa.

Bw. Kiwanuka amesema Jumuiya ya Mashauriano ya Kisheria ya Asia na Afrika inatoa jukwaa kwa nchi wanachama kujadili na kushawishi maendeleo ya sheria za kimataifa, ikiwa ni pamoja na sheria ya bahari, mabadiliko ya tabia nchi, usalama wa mtandao wa Internet, sheria ya biashara ya kimataifa, amani na usalama, na taratibu za kutatua migogoro.

(Wahariri wa tovuti:Song Ge,Zhao Jian)

Picha