99久久国产综合色|国产精品,日韩AV一级特黄无码人妻,91在线视频无码,国产网站久章草在线视频

Kundi la M23 lathibitisha tena ahadi ya kufuata mchakato wa amani

(CRI Online) Septemba 02, 2025

Corneille Nangaa (L), head of the Congo River Alliance, a politico-military coalition allied with the March 23 Movement (M23), speaks at a press conference in Goma, North Kivu Province, the Democratic Republic of the Congo (DRC), on Spet. 1, 2025. The M23 rebel group on Monday reaffirmed its commitment to pursue the peace process under Qatari mediation, despite ongoing differences with the government of the Democratic Republic of the Congo (DRC). (Str/Xinhua)

Corneille Nangaa (kushoto), Mkuu wa Kundi la Muungano wa Mto Kongo, ambalo ni shirika la kisiasa na kijeshi linalohusiana na M23, akiongea kwenye mkutano na waandishi wa habari huko Goma, Jimbo la Kivu Kaskazini, DRC, Sepemba 1, 2025. (Str/Xinhua)

Kundi la M23 jana Jumatatu lilithibitisha tena dhamira yake ya kuendeleza mchakato wa amani chini ya upatanishi wa Qatar licha ya tofauti zinazoendelea na serikali ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC).

Mkuu wa Kundi la Muungano wa Mto Kongo (Congo River Alliance), mshirika wa M23, Bw. Corneille Nangaa akizungumza na wanahabari mjini Goma amesema ana imani na juhudi za upatanishi za Qatar.

Kauli hiyo imetolewa wakati ambapo serikali ya DRC na kundi la M23 yamerejesha mazungumzo huko Doha, ikifuata kanuni zilizosainiwa tarehe 19 Julai ya kupanga kuanzisha mazungumzo kabla ya tarehe 8 Agosti na kufikia makubaliano ya amani ifikapo tarehe 18 Agosti. Licha ya kwamba hatua hiyo haijafikiwa, Doha inasalia kuwa jukwaa pekee la mazungumzo ya moja kwa moja kati ya pande hizo mbili katika wiki za hivi karibuni.

(Wahariri wa tovuti:Song Ge,Zhao Jian)

Picha