

Lugha Nyingine
Serikali ya Ghana yaimarisha usalama katika mkoa wa Savannah ili kutatua mgogoro wa kikabila
(CRI Online) Septemba 01, 2025
Serikali ya Ghana imetoa taarifa ikisema imetuma askari polisi na wanajeshi zaidi katika mkoa wa Savannah nchini humo ili kurejesha utulivu na kusimamisha mapigano ya kikabila kati ya makundi mawili.
Taarifa hiyo imesema waziri wa mambo ya ndani pia ameongoza ujumbe wenye mamlaka ya juu kukutana na viongozi wa makabila ili kujadili hatua za kusimamisha mapigano.
Mapigano makali ya kugombea ardhi kati ya makabila ya Brifo na Gonja yaliyotokea wiki moja iliyopita yamesababisha vifo vya watu 20 na wengine mamia kujeruhiwa, na zaidi 1,000 wamekimbia makazi yao, huku mashamba, maduka na biashara vikitelekezwa au kuharibiwa.
(Wahariri wa tovuti:Song Ge,Zhao Jian)
Kuhusu Tovuti ya Gazeti la Umma
people.cn © Tovuti ya Gazeti la Umma
people.cn © Tovuti ya Gazeti la Umma