99久久国产综合色|国产精品,日韩AV一级特黄无码人妻,91在线视频无码,国产网站久章草在线视频

UNESCO yazindua safari ya Mlima Kilimanjaro ili kuongeza uelewa wa kuyeyuka kwa barafu

(CRI Online) Agosti 06, 2025

Shirika la Elimu, Sayansi na Utamaduni la Umoja wa Mataifa (UNESCO) imesema, safari ya watu 50 kupanda Mlima Kilimanjaro inaendelea ili kuongeza uelewa kuhusu kuyeyuka kwa haraka kwa barafu kunakosababishwa na mabadiliko ya tabianchi.

Mlima Kilimanjaro, ambao umewekwa katika Orodha ya Urithi wa Dunia tangu mwaka 1987 na chanzo muhimu cha maji kwa mamilioni ya Wakenya na Watanzania, unapoteza barafu yake kwa kasi kubwa.

Vijana kutoka Kenya, Tanzania, Marekani, wanasayansi, wataalamu wa Umoja wa Mataifa, na wanaharakati wa mazingira wameanza kupanda mlima huo Jumatatu wiki hii, ili kuelekeza macho ya jamii ya kimataifa kuhusu tishio hilo.

UNESCO imesema, tangu mwaka 1912, Mlima Kilimanjaro umepoteza asilimia 85 ya barafu yake na zaidi ya asilimia 30 ya msitu wake.

(Wahariri wa tovuti:Song Ge,Renato Lu)

Picha