99久久国产综合色|国产精品,日韩AV一级特黄无码人妻,91在线视频无码,国产网站久章草在线视频

Wataalamu waonya mgawanyiko wa Sudan wakati juhudi za amani zikikwama

(CRI Online) Agosti 06, 2025

Wachambuzi wameonya kuwa, mgogoro wa Sudan una hatari ya kuleta mgawanyiko usioweza kusuluhishwa, wakati juhudi za kidiplomasia zikishindwa na mgawanyiko wa ndani ukiongezeka.

Mpaka sasa, Jeshi la Sudan limepata mafanikio makubwa katika maeneo ya mashariki na katikati ya Sudan, likichukua udhibiti wa maeneo muhimu ikiwemo mji mkuu wa nchi hiyo, Khartoum, wakati RSF likidhibiti sehemu kubwa za magharibi na kusini mwa nchi hiyo, ikiwemo mikoa ya Darfur na Kordofan Kusini.

Sudan imeendelea kukabiliwa na mapigano makali kati ya jeshi la nchi hiyo na kikosi cha RSF yaliyoanza mwezi April, 2023, na kusababisha vifo vya maelfu ya watu na wengine mamilioni wakikosa makazi na kuwa wakimbizi wa ndani na nje ya nchi hiyo, na kuongeza mgogoro mkubwa wa kibinadamu nchini humo.

(Wahariri wa tovuti:Song Ge,Renato Lu)

Picha