99久久国产综合色|国产精品,日韩AV一级特黄无码人妻,91在线视频无码,国产网站久章草在线视频

Kenya kuwa mwenyeji wa maonesho ya kilimo ili kuimarisha uhusiano wa kibiashara kati ya China na Afrika

(CRI Online) Julai 30, 2025

Kenya imepangwa kuwa mwenyeji wa Maonesho ya Kimataifa ya Kilimo ya Afrika (AIAE) 2025 mwezi Oktoba, yakilenga kuimarisha ushirikiano kati ya China na Afrika katika biashara ya kilimo na uwekezaji, waandaaji wa maonyesho hayo wamesema jana Jumanne.

Maonesho hayo yaliyopangwa kufanyika Oktoba 28 hadi 31, yameandaliwa kwa pamoja na Maonesho ya Kimataifa ya Hunan Hongxing na Maonesho ya Kilimo Afrika, kwa uungaji mkono wa Wizara ya Kilimo na Maendeleo ya Mifugo ya Kenya na yatafanyika chini ya kaulimbiu "Kuongeza Tija ya Kilimo Barani Afrika Kupitia Uvumbuzi na Ufikiaji wa Soko".

Akizungumza na wanahabari katibu mkuu wa Wizara ya Kilimo ya Kenya, Paul Kipronoh Ronoh, amesema maonesho hayo yatatoa jukwaa kwa wadau wa Afrika kujaribu na kufahamu teknolojia za kisasa kutoka China na dunia nzima zinazohitajika kuifanya sekta ya chakula katika bara hilo kuwa ya kisasa.

Kwa mujibu wa Ronoh wageni zaidi ya 15,000 wanatarajiwa kushiriki maonesho hayo.

Naye Ding Guiping, naibu meneja mkuu wa Maonesho ya Kimataifa ya Hunan Hongxing, amesema maonesho hayo ya mwaka huu yatavutia ushiriki wa nchi 17 na waonyeshaji wapatao 200, zikiwemo kampuni 100 za China.

(Wahariri wa tovuti:Shixi,Zhao Jian)

Picha