99久久国产综合色|国产精品,日韩AV一级特黄无码人妻,91在线视频无码,国产网站久章草在线视频

Tamasha la “Giants of Africa” laanza nchini Rwanda likichanganya michezo, utamaduni na uongozi

(CRI Online) Julai 28, 2025

(Picha/Xinhua)

(Picha/Xinhua)

Tamasha la “Giants of Africa” la mwaka 2025 limeanza mjini Kigali, nchini Rwanda, siku ya Jumamosi, likiwaleta pamoja vijana na makocha wapatao 400 kutoka kote barani Afrika katika shamrashamra za wiki nzima zinazohusisha mpira wa kikapu, utamaduni, muziki, elimu na uhusiano.

Tamasha hilo linalofanyika chini ya kaulimbiu ya "Afrika Isiyo na Mipaka," linalenga kutumia nguvu ya ushawishi wa michezo ili kuelimisha, kuhamasisha, na kuwezesha viongozi wa kizazi kijacho wa Afrika, huku likihimiza umoja na fursa za kuvuka mipaka.

Mbali na ushiriki wa vijana, tukio hilo pia huwaleta pamoja washauri kutoka kote Afrika na kwingineko, likiunda jukwaa lenye hamasa kwa ajili ya mabadilishano ya ujuzi na ukuaji.

Tamasha hilo limepangwa kuendelea hadi Agosti 2.

(Picha/Xinhua)

(Picha/Xinhua)

(Wahariri wa tovuti:Song Ge,Zhao Jian)

Picha