99久久国产综合色|国产精品,日韩AV一级特黄无码人妻,91在线视频无码,国产网站久章草在线视频

Makamanda wa vyuo vya kijeshi vya Afrika wakutana Rwanda kuimarisha ushirikiano

(CRI Online) Julai 23, 2025

Mkutano wa wakufunzi wakuu kutoka vyuo vya ukamanda na unadhimu vya nchi 18 za Afrika umefunguliwa Jumatatu mjini Kigali, ukilenga kuimarisha ushirikiano kati ya vyuo hivyo na kuboresha ubora na umuhimu wa mafunzo na elimu inayotolewa.

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na Wizara ya Ulinzi ya Rwanda, mkutano huo, utakaofanyika mpaka kesho Alhamisi, unatarajiwa kufikia uelewa wa pamoja kuhusu matishio yanayoibuka na uhalisia wa kioperesheni.

Akifungua mkutano huo, Mnadhimu Mkuu wa Jeshi la Rwanda Mubarakh Muganga amesisitiza umuhimu wa kuwawezesha maofisa wa kijeshi kuwa na viwango vya juu vya kitaaluma na kitaalamu, pamoja na hitaji la kufanya operesheni za pamoja katika kanda tofauti.

Bw. Muganga amerejea tena ahadi ya Rwanda ya kushirikiana na nchi zote wanachama katika kuimarisha ushirikiano, kuwianisha mtaala wa mafunzo, na kuingiza uvumbuzi wa kidijitali kwenye mifumo ya mafunzo ya kijeshi.

(Wahariri wa tovuti:Song Ge,Zhao Jian)

Picha