99久久国产综合色|国产精品,日韩AV一级特黄无码人妻,91在线视频无码,国产网站久章草在线视频

Mashambulizi ya droni katika Bandari ya Sudan yakwamisha usambazaji wa misaada ya kibinadamu

(CRI Online) Mei 08, 2025

Msemaji msaidizi wa Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Bi. Stephanie Tremblay amesema kuwa mashambulizi ya droni katika kituo cha misaada cha mji wa Port Sudan yanakwamisha usafirishaji wa misaada na wafanyakazi wawezeshaji usambazaji.

Bi. Stephanie ameongeza kuwa Shirika la Mpango wa Chakula Duniani (WFP) limesimamisha shughuli zake za kutoa Huduma ya Misaada ya Kibinadamu kupitia Angani kuanzia Jumapili na hazitarejeshwa hadi hali itakapokuwa salama, hali ambayo inazorotesha zaidi utoaji wa msaada unaohitajika haraka.

Naibu Katibu Mkuu wa Masuala ya Kibinadamu Tom Fletcher ameelezea wasiwasi wake mkubwa juu ya mashambulizi hayo ya droni dhidi ya Port Sudan, akisema sheria ya kimataifa ya kibinadamu lazima iheshimiwe na huduma endelevu lazima zitolewe ili kuokoa raia na miundombinu ya kiraia.

(Wahariri wa tovuti:Zhou Linjia,Zhao Jian)

Picha